Kupitia kwenye account yake ya twitter Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Humphrey Polepole ametoa majibu kwa Mbunge wa Iringa Mjini Mchungaji Peter Msigwa akimwambia kuwa hatokuwa tena Mbunge baada ya Awamu hii.
Hatua hiyo ya Polepole imekuja baada ya kuambiwa na Mbunge Msigwa kuwa viatu vya Nape havimtoshi kupitia twitter ambapo aliandika; "Kitendo cha Msukuma kumkumbuka Nape , ni ujumbe tosha Kuwa Viatu vya Nape vinampwaya POLEPOLE!"

Comments
Post a Comment