
Waziri wa mali asili na utalii Prf Jumanne Maghembe ameagiza kukamatwa kwa baadhi ya wamiliki wa hoteli mkoani hapa kwa madai ya wafanyakazi wao kujiingiza katika utapeli kwa kuwarubuni wageni wanaoingia hapa nchi kitendo ambacho ameeleza kuwa kinashusha utalii na kuwafanya wageni kushindwa kutembelea vivutio mbalimbali hapa nchini.
Prf Maghembe ameyasema hay oleo katika mkutano maalumu uliofanyika mkoani Arusha pamoja na wamiliki mbalimbali wa hoteli kutoka mikoa wa Manyara na Arusha ambapo ameeleza kuwa zipo taarifa mbalimbali za wageni kutapeliwa fedha zao ndipo waziri huyo alipotoa agizo hilo.
INSRT MAGHEMBE
Licha ya waziri Maghembe kutoa agizo hilo akazungumzia migogoro ya ardhi Loliondo kati ya wakulima na mamlaka za hifadhi zilizowazunguka.
INSERT MAGHEMBE
Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hifadhi za taifa TANAPA Allan Kijazi ameeleza kuwa suala la udanganyifu katika sekta ya utalii ni miongoni mwa vitu vinavyoharibu sekta ya utalii ambapo hapa anazungumzia juu ya watu ambao wanafanya udanganyifu huo.
INSERT KIJAZI
Kumekuwa na taarifa mbalimbali za wageni kutapeliwa ambapo wapo baadhi ya wageni wliolalamika kurubuniwa ambapo tatizo hilo likafanya waziri huyo kuamua kutoa agizo hilo la kukamatwa kwa watu hao
Comments
Post a Comment